Wednesday, March 13, 2013

HAYA NI MAPITO TU


EEEHHH' MUNGU tusaidieeee''

Siku hizi binadam tumekuwa kama wanyama NA ni afadhali na mara mia ya wanyama na hatuoni thamani tulizonazo hata kufanya yasiyostahili....Hii ni habari ya mda kdg ila katika pitapita zangu kuna rafiki yangu wa karibu alinipa hii ''case'' ya huyu dada jamani kwakweli binadam wa sasa ni wachache wenye huruma na utu.....kweli wapo ila sio wote ni wachache mnooooo,jamani mnooooo'''mh''nilishindwa kuvumilia chozi likanitoka

 

Kwa wewe ambae hukuona ilikua hivi,,,,

undefined

                                                            Sophia rashid
“HAYA ni mapenzi ya Mwenyezi Mungu na si kazi ya binadamu, nasikitika kwa sababu mume wangu amenitelekeza baada ya kuona watoto wamevimba kichwa,” hayo ni maneno yaliyotamkwa na Sophia Rashid , 22, mkazi wa Chanika nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam ambaye anauguza wanaye wawili wanaosumbuliwa na uvimbe wa kichwa.

Mama huyo alisema watoto wake hao aliwazaa wakiwa na matatizo ya kuvimba vichwa kutokana na kujaa maji, hali ambayo inamfanya akose raha.

“Kwangu sasa imekuwa ni matatizo makubwa mwanangu Omari mwenye miaka minne na Maulid mwenye miezi kumi wanasumbuliwa na ugonjwa mmoja ambao umesababisha baba yao kuwakimbia,” alisema mama huyo akiwa katika Taasisi ya Mifupa (Moi)…
Aliongeza kuwa, tangu alipofika hospitalini hapo wiki mbili zilizopita, amekuwa akipata msaada kutoka kwa maofisa wa ustawi wa jamii wa Moi lakini ndugu zake hawafiki kabisa kumjulia hali.
Daktari mmoja hospitalini hapo aliyezungumza kwa sharti la kutoandikwa jina gazetini alisema kuwa, hali hiyo huwapata watoto kutokana na kuwa na upungufu wa madini ya pholic acid na mjamzito kukosa lishe bora wakati wa ujauzito.
MSAADA
Kutokana na matatizo hayo mama huyo anaomba kusaidiwa na mtu yeyote aliyeguswa na masaibu yake kifedha, chakula, mavazi, dawa pamoja na kipimo cha TC Scan ambacho alidai kuwa kipo katika Hospitali ya Regency ya jijini Dar es Salaam na gharama yake ni shilingi 258,000 kwa mtoto mmoja.
Atakayependa kumsaidia mama huyo atumie simu namba 0716755384 au afike Hospitali ya Muhimbili, Moi kwenye wodi A.

  HUU ni msalaba wa mwenzetu Sophia ila kiuhalisia wote tunapaswa kuona ugumu alionao'Hii ni pesa ndogo ambayo kwa mtu na uwezo wake anaweza fanya bila hata kuwaza au kufikiria mara mbili jamani ......Ni  jukumu la wenye nacho au wasionacho kusaidia kwa nafasi yoyote mtu unaweza msaidia mwanamke mwenzetu Na MUNGU atakuongezea kwa ulichotoa coz naamini kuna watu kama hawa sehem fulani wanahitaji kusikia japo neno la faraja tu hawalipati so nahisi tunaweza fanya kitu kwaajili yake.

  

 '''SAD NEWS'''

NILIFANYA JITIHADA ZA KUMTAFUTA 

Nilifanikiwa kumpata na habari ya kusikitisha ambayo niliyokutana nayo aliniambia tayari watoto hawa wamefariki dunia na hata arobaini yao bado na msiba ulikua nyumbani kwao chanika.......iliniuma na kusema bado Mungu anapaswa ashukuriwe kwa kila jambo yeye ana makusudi juu ya maisha ya sophia kama ilivyo kwangu na kwako.'Bwana ametoa,bwana ametwaa,jina lake lihimidiwe''

 

MUHIMU

Sihitaji kupokea pesa yoyote ila tutachokifanya kila mtu kwa nafasi yake au km group kwa wale watakaokua tayari kusaidia kupanga siku tukapata mda mfupi tu  tukamtembelee na itategemea tutakavyoamua na kumtia moyo'au unaweza kuwasiliana nae na kujua vp unaweza kumfikia na kumpatia pole yako kwa matatizo haya yaliyompata.

    

Huyu dada alitoa namba yake hapo juu na NAWIWA KUSEMA binafsi nahisi kufanya chochote kidogo kwa ajili yake hata kama ni kidogo,kama unatamani kuungana na mm ktk hili tuwasiliane na tujue nn cha kufanya ili tujitoe kwa ajili yake hata kidogo,,,,nasisitiza hata kidogo usijidharau amini wewe ni msaada wa mtu fulani mahali popote ulipo sio lazima pesa ni chochote........TUWASILIANE KWA

 0714 950054,0754207238 au bkanemba@yahoo.com

   

MUNGU AKUBARIKI SANA''