Thursday, December 20, 2012

MCH.KANEMBA ANAKUALIKA


   UNGANA NA MCHUNGAJI KANEMBA KATIKA MAOMBI YA DUNIA
Mchungaji Kiongozi wa kanisa la TAG Magomeni ambaye yuko South afrika Kwa masomo, ameanzisha mtandao wa maombi kwa njia ya skype. maombi hayo ambayo yameanza mwezi uliopita yamekuwa ya baraka sana kwa wanaoshiriki. akiongea kutoka UK Bonny Shauri amefurahi jinsi technolojia inavyowezesha watu kutoka pande tofauti za Dunia kufanya maombi ya pamoja, maombi hayo yanayoongozwa na mchungaji huyo yanalenga sana mahitaji muhimu ya kila siku kama ifuatavyo
1. Afya 
2. Taifa (Serikali)
3. Kanisa 
4. Uamsho
5. Mafaniko kiuchumi na baraka za ndoa na watoto

kwa sasa ambao wameweza kujiunga na mtandao huu wa maombi ya  live ni Familia ya Silomba iliyoko Marekani, Familia ya Bonny Shauri Iliyopo UK, Ndugu Japhet aliyeko Sweden, Martin Malecela Tazania, Issack Kisiva Tanzania, Joseph Mwakibuti Tanzania, Peace Lumelezi na Charles Mwaihojo Tanzania na yanaongozwa na mch akiwa south Africa. maombi hayo ambayo yanafanyika kila jumamosi usiku kuanzia saa 22:00 kwa saa za Tanzania. Mchungaji Kanemba ameomba watu mbalimbali kujiunga ili tuweze kuomba kwa pamoja maana ni njia mojawapo ya kusababisha mafanikio katika familia zetu, maombi hayo ambayo huanza na neno linalotolewa na mch halafu maombi na kama kuna mtu mwenye hitaji binafsi basi baada ya maombi anaweza kuwasiliana na Mch kwa maombi na ushauri zaidi kwa njia hiyo ya skype.



hakika hakuna linaloshindikana mbele zake mungu...katika umbali wowote mungu anafika na  kukujibu haja ya moyo wako






































No comments: