Thursday, December 20, 2012

AMELAANIWA MTU YULE AMTEGEMEA MWANADAMU

Nguzo ya siku'''''''

IMANI YAKO ikimgusa MUNGU hautabaki kama ulivyo

                    Leo nawakumbusha wapendwa kuhusu kumtegemea MUNGU, na kumtumaini yeye kama BWANA NA MWOKOZI

 (ISAYA51;7)Amebarikiwa mtu yule amtumainiye BWANA, kwa maana hiyo kuna baraka katika kumtumaini BWANA, lakini kuna laana katika kumtumaini mwanadamu kama kinga(ISAYA51;5),

Usimtumaini mwanadamu MUNGU hapendi wewe umpe utukufu mwanadamu, hebu litaje jina la BWANA kila wakati, usitaje mali uliyonayo haitakusaidia(ZABURI 20;7) hawa wanataja farasi na hawa magari lakini sisi tutalitaja jina la BWANA.Hata kama unataka pesa hebu litaje jina la BWANA kwani amesema pesa na dhahabu ni za BWANA(HAGAI 2;8)










































No comments: