Friday, December 21, 2012

VIONGOZI WA CHAMA CHA INJILI WAPATIKANA RASMI

Ni katika  Hotel ya Wanyama iliyoko Sinza Mori kumefanyika kongamano la waimbaji wa Muziki wa Injili lililo andaliwa na chama cha Muziki wa Injili Tanzania "CHAMUTA" 
 limefanyika likiwa na lengo la kutambulisha viongozi wapya wa chama cha muziki wa Injili Tanzania.

Katika kongamano hilo lilihudhuriwa na Mfuko wa pensheni wa LAPF.Mfuko huu ulizungumzia umuhimu kwa waimbaji wa muziki wa injili kujiunga nao kama sehemu mojawapo ya wao kuwekeza katika maisha ya baadae,pia kutoa fursa kwao kujipatia mikopo ya nyumba na kuwekeza katika akiba yao ya baadae.  

Pichani ni baadhi ya matukio katika kongamano hilo


Mwanamuziki mkongwe wa injili UPENDO KILAHIRO akiongea katika kongamano hilo katika Hoteli ya wanyama sinza


Mwimbaji wa muziki wa injili BAHATI BUKUKU akisikiliza kwa makini wakati wa kongamano hilo



                           Mwimbaji mkongwe nchini mzee Makasy akiandika point muhimu

               Pastor Abel Orgenes ambaye amekuwa karibu sana na waimbaji wa gospel


                 Comedian King Chavala alikuwepo kujua umuhimu wa chama hicho

 Hapa ni mwimbaji maarufu Addo November Mwasongwe Rais wa chama cha wasanii akiwa na mkurugenzi wa Grace Product.

PICHANI CHINI............

           Abubakar Ndwaka meneja mafao wa LAPF akizungumza jambo katikakongamano hilo

No comments: